Waziri wa madini na uchumi samawati Salim Mvurya amesema kuwa serikali inapanga kufanya uvuvi kuwa mojawapo ya sekta za uwekezaji.
Akizungumza katika hafla iliyoandaliwa katika taasisi ya uvuvi na utafiti wa baharini KMFRI, Mvurya amesema muda umewadia kwa wavuvi kujisajili kama vyama vya ushirika ili kufaidika na miradi iliyowekwa na serikali katika sekta ya uvuvi.
Waziri huyo amesema kuwa serikali imetoa shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya mpango huo.
Vile vile Mvurya amesema serikali inalenga kuimairisha miundo msingi katika maeneo yaliyo na bahari au mito ili kuimarisha sekta ya uvuvi
Aidha amewataka viongozi katika sekta ya uchumi samawati kujukumika katika majukumu waliyopewa.


 

More Stories

Vita dhidi ya mihadarati vyapamba moto Pwani

Fuo za bahari sasa ni marufuku

Ufunguzi wa shule waahirishwa kwa muda usiojulikana

Buriani jenerali Francis Ogolla