Serikali ya kitaifa na kaunti zatakiwa kushirikiana kuwawezesha wavuvi kwa vifaa vya kisasa

Ipo haja ya serikali ya kitaifa na zile za kaunti kushirikiana kuhakikisha inawekeza zaidi kwa kuwawezesha wavuvi kupata vifaa kuvua katika bahari kuu.Gavana wa Lamu Issa Timamy ambaye pia ni...

Kongamano la kujadili uchumi wa baharini lakamilika huku hamasisho zaidi zikitolewa kupiga jeki juhudi hizo

Kongamano la kujadili mbinu za kuboresha uchumi wa baharini baina ya mataifa wanachama wa IGAD limekamilika rasmi hapa jijini Mombasa.Kongamano hilo la siku nne liliwaleta pamoja wawakilishi kutoka...

Vita dhidi ya mihadarati vyapamba moto Pwani

Fuo za bahari sasa ni marufuku

Buriani jenerali Francis Ogolla

Rais William Ruto atafanya ziara yake ya kwanza rasmi kama Rais wa tano Pwani wiki hii baada ya kuagiza kwamba huduma za bandari zirejeshwe katika bandari ya Mombasa.

Tamko hilo limepokelewa kwa furaha na washikadau ambao wamemshukuru Dkt Ruto kwa kutimiza ahadi yake ya kampeni kwa kubatilisha agizo lililotolewa na aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta.

Uhamisho wa huduma za bandari kutoka Mombasa hadi Bohari ya Kontena ya Nairobi na Naivasha ilikuwa mada kuu katika kampeni za urais katika kaunti za Mombasa na Nakuru.

Viongozi kutoka Mombasa wamekuwa wakiunga mkono kurejea kwa shughuli za bandari katika mji wa pwani, huku wenzao wa Nakuru wakishinikiza uwekezaji zaidi katika ICD ya Naivasha.

Wadau wa bandari wamekaribisha agizo la Dkt Ruto, wakisema hatua hiyo itafufua uchumi.


RadioRahma ads